NIDA Yazindua Mfumo wa Kujua Kilipo Kitambulisho

Na Calvin Minja – NIDA

Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) imezindua mfumo mpya wa kidigitali unaomuwezesha mwananchi kujua kitambulisho chake kipo eneo gani kwenye Wilaya aliojiandikisha.

Mfumo huo ni mahususi kwa wananchi wote ambao wamejiandikisha na bado hawajachukua Vitambulisho vyao katika Ofisi za NIDA za Wilaya.

Mfumo huu umekuja baada ya NIDA kuzindua zoezi la ugawaji Vitambulisho kwa Umma, zoezi hilo lilizinduliwa Kitaifa Oktoba 12, 2023 mkoani Mara na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (Mb).

Zoezi la ugawaji wa Vitambulisho kwa umma kwa mkupuo linatagemea kuhitimishwa mwezi Machi, 2024 ambapo kila aliejiandikisha atakuwa amepata Kitambulisho chake.

Huduma hii ya kujua Kitambulisho kilipo inapatikana kwa kupitia tovuti ya Mamlaka www.nida.go.tz kisha utabofya mahali palipoandikwa Kitambulisho cha Taifa ikifuatiwa na palipoandikwa Fahamu Kitambulisho kilipo, au kwa kufungua kiunganishi wezeshi http://vitambulisho.nida.go.tz kisha utachagua Mkoa ambao ulijiandikisha, utachagua Wilaya uliojianikisha na mwisho utachagua jina la Kijiji au Mtaa uliojiandikishia na kuangalia jina lako  kwenye orodha kama halitakuwepo utatakiwa kufika kwenye Ofisi ya NIDA ya Wilaya ulipojiandikisha kujua kuna changamoto gani kwenye maombi yako.

“Lengo la kuanzisha mfumo huu ni kurahisisha upatikanaji wa huduma na kumrahisishia mwananchi kujua wapi kitambulisho chake kilipo bila kufika kwenye Ofisi zetu. Nitoe rai kwa wananchi kuchukua Vitambulisho vyao kwa  wakati katika Ofisi za Serikali ya Mtaa/Kijiji walichojiandikisha ndani ya muda uliopangwa  pia kuwapatia ushirikiano wadau wote wanaohusika kwenye zoezi hili   ” Geofrey Tengeneza, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano NIDA.

Mpaka sasa NIDA imepokea jumla ya maombi  24,495,804 ya watu wanaohitaji Utambulisho wa Taifa pamoja na Kitambulisho cha Taifa, jumla ya Namba za Utambulisho wa Taifa zilizozalishwa mpaka  sasa ni  20,786,171, Vitambulisho ambavyo vimeshazaliswa ni 19,370,666 jumla ya Vitambulisho vilivyosambazwa ni 17,161,600 na  Vitambulisho ambavyo vimechukuliwa ni  12,837,523.

Kwa upande mwingine NIDA tayari ilikwisha zindua usajili kwa njia ya mtandao ambapo muombaji anatakiwa kuingia kwenye kiunganishi wezeshi cha https://eonline.nida.go.tz kisha kutafuata maelekezo. Huduma nyingine inayopatikana kwa njia ya mtandao ni  huduma ya kuangalia namba ya Utambulisho wa Taifa ambapo mwananchi anafungua kiunganishi wezeshi https://services.nida.go.tz/nidportal/get_nin.aspx kisha anajaza taarifa zake kwa usahihi na kubonyeza neno tuma.

Comments on “NIDA Yazindua Mfumo wa Kujua Kilipo Kitambulisho”

  1. Henelko Pius says:

    1. Naomba kuuliza kwamba endapo kwa bahati mbaya mda wa mwisho wa kuchukua kitambulisho cha taifa kwenye wilaya ulipojiadikishia utaisha kabla hakijachukuliwa, mwanainchi atafanya nini ili kupata kitambulisho chake ?
    2. Je? Ninaweza kumuagiza mtu kunichukulia kitambulisho cha taifa

    1. Geofrey Tengeneza says:

      Salaam Ndg.

      Muda wa kuchukulia Serikali za Mitaa ukiisha, Vitambulisho vinarudishwa kwenye ofisi ya Usajili wilayani ulikosajiliwa.
      Utaratibu wa sasa kwa wanaoruhusiwa kucukilia/wa ni watoto nawazazi, wagonjwa, wazee, wanandoa ama kwa ambao mwenekiti amejiridhisha kuwafahamu. Anayemtuma mtu ataandika barua na anayemchukulia mtu ataandfika barua ya kukiri kumchukulia mtumaji.

      Shukrani.

      1. Henelko Pius says:

        Axante kwa mrejesho

    2. Amed Wilson says:

      Hiyo link ya kujua vitambulisho vilipo nayo haifunguki

      1. Geofrey Tengeneza says:

        Mbona inafunguka?

  2. Yunis Oscar fungo says:

    Samahani, nilijiandikisha zaidi ya mwenzi sasa lakini namba haitoki na kila taarifa iko sahihi . Nifanye nini na Nina uharaka sana na Nida number? Nimejaribu kurudi nilipojiandikisha bado nikaambiwa nisibiri zaidi, nimejaribu kutuma ujumbe lakini hakuna majibu yeyote.. naomba mnisaidie niipate Kwa wakati au nielezwe nifanye nini’ Asante

    1. Geofrey Tengeneza says:

      Tafadhali fungua link https://services.nida.go.tz kisha chagua Fahamu NIN kujua namba yako

  3. Happines. Marko says:

    Habar ivi nida inatumika Kama bima ya afya, na Kama mtu anayo namba ya nida kadi ilipotea afanyaje kupata hiyo kadi

    1. Geofrey Tengeneza says:

      report ya polisi kisha nenda nayo Ofisi yoyote ya NIDA wilaya iliyo karibu na wewe kwa maelekezo na taratibu zaidi ili kuchapishiwa kingine

  4. catherine nchimbi says:

    Naomba kufahamu namna ya kupata kitambulisho Cha nida
    Ni miaka sita sasa sijapata

    1. Geofrey Tengeneza says:

      Fungua link https://vtambulisho.nida.go.tz kufahamu kitambulisho kilipo

  5. Emily Emmanuel says:

    Samahani ndg
    Huduma ya kuangalia kitambulisho cha nida kama nimeshatoka na mahali kilipo kwa sasa imesitishwa ??

    1. Geofrey Tengeneza says:

      Fungua link https://vtambulisho.nida.go.tz kufahamu kitambulisho kilipo

  6. Christian Mabonesho says:

    Napata wapi kitambulisho
    Maaana wenzangu wamepata mm mpaka hatua hii sijakipata
    Na selikali za mitaaa akipo kama kipo tayar naeza kifata gongol la mboto
    Kwa kituo cha nida?

    1. Geofrey Tengeneza says:

      Tafadhali Fungua link https://vitambulisho.nida.go.tz kujua kitambulisho chako kilipo

  7. Ibraim Mwakyambo says:

    Habari za majukumu waheshimiwa!
    Nanba ya kitambulisho changu nimeipata tangu mwaka 2022, lakini kwa bahati mbaya jina langu la kwanza limekosewa herufi moja IBRAHIM badala ya IBRAIM yaani herufi H ndiyo inayotakiwa kutoka, Na kitu kingine kilichokosewa ni tarehe ya kuzaliwa 08/12/…., badala ya tarehe 18/12/…., kama ilivyo kwenye cheti cha kuzaliwa.
    naomba nisaidiwe katika hili kwasababu taarifa za namba yangu ya NIDA hazifanani na taarifa zangu za elimu.
    Nasubili mrejesho nikiwa na tumaini la kusaidiwa kwa haraka.
    Ahsante!

    1. Geofrey Tengeneza says:

      Nenda Ofisi ya NIDA wilayani kupata maelekezo na taratibu za mabadiliko ya taarifa

  8. Juma says:

    Habari najaribu kuangalia namba yangu ya nida online nikafanikiwa kuiyona ila nilikuwa sijai copy sehemu yeyote saizi najaribu kuangalia Tena nashindwa kuipata sijajua tatizo nini wakati taarifa zangu nilizo angalia mwanzo namba yangu ya nida ndio hizo hizo zinazo kataa

    1. Geofrey Tengeneza says:

      Tafadhali fungua link https://services.nida.go.tz kisha chagua fahamu NIN na kufuata maelekezo kujua namba yako

  9. Heppyfania Emmanuel Ngoye says:

    Hbr Ndg…pole pia na majukumu naomba kufahamu namna ya kujua kitambulisho kilipo?

    1. Geofrey Tengeneza says:

      Tafadhali fungua link https://vitambulisho.nida.go.tz kujua kitambulisho chako kilipo.

  10. Zubeda Ibrahim says:

    Sorry naomba kufahm kitambulish changu kilipo mpak mda huu na nilisikia vimetokasijapata

    1. Geofrey Tengeneza says:

      Tafadhali fungua link https://vitambulisho.nida.go.tz kisha fuata maelekezo kufahamu kitambulisho chako kilipo

  11. Zubeda Ibrahim says:

    Nahitaj kufahm kitambulish changu sijakipata toka mwak jana

    1. Geofrey Tengeneza says:

      Tafadhali fungua link https://vitambulisho.nida.go.tz kisha fuata maelekezo kufahamu kitambulisho chako kilipo

    1. Geofrey Tengeneza says:

      Karibu tukuhudumie

  12. Mwagala mbusi nyanza says:

    Ninaitwa mwagala mbusi nyanza nimzaliwa wa kilimanjaro wilaya ya hai kata ya boma ng,ombe kitongoji cha kibaoni nilijisajili katika kupata kitambulisho cha taifa katika mkoa kilimanjaro wilaya yahai nilikua nauliza ninaweza kukipata kitambulisho cha taifa kwanjia ya simu

    1. Geofrey Tengeneza says:

      Hapana, kifuate sehemu kilipo ili ukachukue

  13. Stanley makelele kubita says:

    Kwanini naingia kwenye mfumo wa kuangalia kitambulisho kilipo lakini inakataa kufunguka page

    1. Geofrey Tengeneza says:

      inawezekana ni shida ya mtandao, endelea kfungua

  14. Revocatus Mang'wata says:

    Mimi nikujaza taarifa zangu, nikituma inaniambia jaza taarifa zako kwa usahihi, nahitaji msaada.

    1. Geofrey Tengeneza says:

      Maana yake kuna kitu unakosea, hasa herufi za majina yako na ya mama.

  15. Israel Laizer says:

    Nataka kitambulisho changu

    1. Geofrey Tengeneza says:

      Fungua link ifuatayo: https://vitambulisho.nida.go.tz kufahamu kitambulisho kilipo

  16. gift urio says:

    Nilifanikiwa kupata namba yangu ya nida na niliitumia sehemu mbalimbali, lakini kwa sasa kila nikiitumia naambiwa haipo shida itakuwa ni nini?

    1. Geofrey Tengeneza says:

      Tafadhali tembelea Ofisi yoyote ya NIDA eleza shida hiyo kujua tatizo ni nini na utahudumiwa ipasavyo

  17. Gift urio says:

    Kila nikitumia namba yangu ya nida naambiwa haipo kwa sasa shida itakuwa ni ni i?

    1. Geofrey Tengeneza says:

      Tafadhali tembelea Ofisi yoyote ya NIDA eleza shida hiyo kujua tatizo ni nini na utahudumiwa ipasavyo

  18. ANNA DALTON TARMO says:

    Nimefuata kitambulisho changu mahali nilipojiandikisha na taarifa zinaonesha kuwa kitambulisho kilishatoka maana nimejiandikisha 2017 na hakijulikani kilipo nitafanya Nini ili kukipata na Kama nitashindwa ni njia gani mbadala wa kupata kitambulisho changu?

    1. Geofrey Tengeneza says:

      Tafadhali fungua link ifuatayo https://vitambulisho.nida.go.tz ili kufahamu kitambulisho chako kilipo

  19. Joseph ikombe katambi says:

    Naitwa Joseph ikombe katambi naulizia kitambulisho changu Cha NIDA

    1. Geofrey Tengeneza says:

      Fungua link ifuatayo: https://vitambulisho.nida.go.tz kisha fuata maelekezo au piga simu 0232210500 kufahamu Kitambulisho kilipo

  20. Essau Daudi Ntandu says:

    Jamani mbona izo link za kuangalia vitambulisho kama vimetoka hazifunguki?

    1. Geofrey Tengeneza says:

      Itakuwa shida ya mtandao. endelea kufungua

  21. Patrick bwire says:

    Nimejiandikisha Zaidi ya Miaka 4 ,nishapata Namba tu lakini kitambulisho nishafatulia hakijatoka lakin Namba inaonyesha taarifa zangu sahihi sasa sijajua tatizo Ni nini?

    1. Geofrey Tengeneza says:

      Tafadhali fungua link https://vitmbulisho.nida.go.tz kisaha fuata maelekezo au piga simu namba 0232210500 kufahamu kitmbulisho chako kilip

  22. Deborah Rweyemamu says:

    Samahan mm nilikuwa naulizia kama mtu majina yake yamekosewa kwenye kitambulisho Cha nida anaweza kwenda kufanya marekebisho?

    1. Geofrey Tengeneza says:

      Ndio unaweza kufanya marekebisho. kama umeshachukua kitambulisho nenda ofisi yoyote ya NIDA wilaya iliyo karibu na wewe na kama kitambulisho bado hakijatoka nenda ofisi uliyojisajilia kwa maelekezo zaidi.

  23. Agripa timoth says:

    Habari, samahani kitambulisho changu ofisi nilipojiandikishia hakipo ila nikiangalia kwa njia ya mtandao wa nida online naambiwa kipo ofisi nilipojiandikishia, kwanini ilihali napo hakipo?

    1. Geofrey Tengeneza says:

      Tembelea Ofisi ya NIDA wilaya uliyojiandikishia kwa usaidizi zaidi

  24. Iddikabuji says:

    Nahitaji kujuwa kama kitamburisho changu kimetoka

    1. Geofrey Tengeneza says:

      Tafadhali fungua link https://vitmbulisho.nida.go.tz kisaha fuata maelekezo au piga simu namba 0232210500 kufahamu kitmbulisho chako kilip

  25. Clinton stivin uronu says:

    Nashindwa kupata kitambulisho changu

    1. Geofrey Tengeneza says:

      Tafadhali fungua link https://vitmbulisho.nida.go.tz kisaha fuata maelekezo au piga simu namba 0232210500 kufahamu kitmbulisho chako kilipo

  26. LETICIA PHILIBERT LUCAS says:

    Naomba msaada, nilijiandikisha na kukamilisha hatua ya kupigwa picha Wilaya ya Itilima kata ya Mwamtani lakini mpaka Sasa sijapata NIN na nimeshahamia mkoa mwingine, je ninaweza kujiandikisha upya?
    Au nifanyeje ili nijue NIN yangu Kama imeshatoka au la!

    1. Geofrey Tengeneza says:

      Tafadhali usijiandikishe tena. fungua link https://services.nida.go.tz kisha fuata maelekezo au piga simu namba 0232210500 kupata msaada zaidi

  27. ABUBAKARI says:

    Nimeshapata kitambulisho Chang lkn Saini haikutoka km nlivyoandika je kuna uwezekano wa kubadilisha

    1. Geofrey Tengeneza says:

      Tafadhali tembelea Ofisi ya NIDA wilaya iliyo karibu nawe kwa maelekezo zaidi

  28. Joel M. Asiago says:

    Samahani mimi nilijiandikisha mweZi wa tano mwaka huu mpaka sasa namba ya NIDA sijapata.naomba kuelewshwa kinachoendelea.

    1. Geofrey Tengeneza says:

      Tafadhali fungua link https://services.nida.go.tz kisha fuata maelekezo au piga simu namba 0232210500 kupata msaada zaidi

  29. Saluleon5@gmail.com says:

    Kujua kitambulisho kilipo mbn haifunguki muheshimiwa au imesitishwa

    1. Geofrey Tengeneza says:

      Itakuwa ni shida ya mtandao tu

  30. Emmanuel azael mauki says:

    Naitaji kujua kitambulisho change kama tayr kwasababu inaenda mwezi wa tatu tangu nijisajiriii na kupata namb ya nida mkuu

    1. Geofrey Tengeneza says:

      Fungua link https://vitambulisho.nida.go.tz kisha fuata maelekezo au piga simu namba 0232210500 kufahamu kama kimetoka na mahali kilipo

  31. David Andrew Butawantemi says:

    Naomba kuona kitambulisho changu cha NIDA

    1. Geofrey Tengeneza says:

      Hatujakuelewa, unahitaji huduma gani ndugu tukuhudumie

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Ukurasa wetu wa Facebook

Ramani ya Ofisi Zetu