emblem

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa

Jisajili, Tukutambue, Tukutambulishe
Mabadiliko ya Taarifa Kundi la watumishi wa umma/watumishi wa umma waliostaafu

Taarifa za Mtumishi wa umma ambazo zinaweza kurekebishwa ni zile ambazo hazitaathiri utambulisho wake wa hapo awali na zitazingatia mambo yafuatayo; -

(i) Makosa yaliyofanywa na Watendaji wa Mamlaka katika utendaji wao wa kazi hususan kwenye marekebisho ya herufi,

(ii) Majina ambayo yameandikwa katika mpangilio wa tofauti (vice versa) na yote yapo katika sehemu ya majina husika,

(iii) Majina ya Mwombaji ambaye alijiandikisha kwa kutumia majina ya mwenza wake baada ya kuolewa na kwa kutoa uthibitisho wa cheti cha ndoa,

Mabadiliko ya Umri kwa kundi la watumishi wa umma/watumishi wa Umma waliostaafu

a) Barua ya utambulisho kutoka kwa Mwajiri wa Mwombaji ikithibitisha taarifa za maombi husika,

b) Kibali kutoka kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma akiridhia mabadiliko husika,

c) Cheti cha kuzaliwa cha mwombaji chenye taarifa ya taarifa hijajika,

d) Afisa Usajili Wilaya anaweza akaomba nyaraka zozote zaidi ambazo ataona zinafaa kuthibitisha taarifa/majina ya mwombaji husika,

e) Mabadiliko yoyote ambayo hayana ushahidi wa nyaraka sahihi katika kuthibitisha maombi ya taarifa husika hayawezi kuruhusiwa/kupokelewa au kuyafanyiwa kazi na watendaji wote,

f) Iwapo makosa yamefanyika upande wetu, Afisa Usajili atajiridhisha na kuendelea na maboresho pasipo mwombaji kulazimika kulipia gharama yoyote lah utapaswa kulipia shilingi 20,000/=,

g) Ombi la mteja litawasilishwa kwenye kamati ya Usajili na Utambuzi wa watu, iwapo watajiridhisha kuwa ombi limekidhi vigezo ndipo watatoa kibali ili Afisa Msajili aweze kuendelea na hatua ya kufanya maboresho, ombi lisipokidhi vigezo, kibali hakitatolewa na Afisa Msajili haruhusiwi kuendelea na hatua yoyote ya maboresho.

Mabadiliko Majina kwa kundi la watumishi wa umma/watumishi wa umma waliostaafu

a) Barua ya utambulisho kutoka kwa Mwajiri wa Mwombaji ikithibitisha maombi ya kubailisha taarifa za maombi husika,

b) Kibali kutoka kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma akiridhia mabadiliko husika,

c) Afisa Usajili Wilaya anaweza akaomba nyaraka nyingine yoyote atakayoona inafaa kuthibitisha taarifa/majina ya Mwombaji.

d) Kata hati ya kiapo cha kubadili jina (Deedpoll) toka kwa wakili anayetambuliwa na Chama cha Mawakili Tanzani (TLS) kisha kiwasilishe Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi ili kupata Usajili wa Jina unalorekebisha kisha ambatanisha kwa pamoja na risiti ya malipo husika,

e) Toa Tangazo kwenye Gazeti la Serikali linalotolewa na Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali kuonyesha mabadiliko ya jina yaliyofanyika,

f) Mabadiliko yoyote ambayo hayana ushahidi wa nyaraka sahihi katika kuthibitisha maombi ya taarifa husika hayawezi kuruhusiwa/kupokelewa au kuyafanyiwa kazi na watendaji wote,

g) Iwapo makosa yamefanyika upande wetu, Afisa Usajili atajiridhisha na kuendelea na maboresho pasipo mwombaji kulazimika kulipia gharama yoyote lah utapaswa kulipia shilingi 20,000/=,

h) Ombi la mteja litawasilishwa kwenye kamati ya Usajili na Utambuzi wa watu, iwapo watajiridhisha kuwa ombi limekidhi vigezo ndipo watatoa kibali ili Afisa Msajili aweze kuendelea na hatua ya kufanya maboresho, ombi lisipokidhi vigezo, kibali hakitatolewa na Afisa Msajili haruhusiwi kuendelea na hatua yoyote ya maboresho,

Mabadiliko ya Majina Kutokana na Kuolewa au Kuachika kwa kundi la watumishi wa umma/watumishi wa umma waliostaafu

a) Barua ya utambulisho kutoka kwa Mwajiri wa Mwombaji ambayo inathibitisha taarifa za maombi husika,

b) Kibali kutoka kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma akiwa amekubaliana na kuriridhia mabadiliko husika,

c) Cheti cha Ndoa/Talaka,

d) Kata hati ya kiapo cha kubadili jina (Deedpoll) toka kwa wakili anayetambuliwa na Chama cha Mawakili Tanzani (TLS) kisha kiwasilishe Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi ili kupata Usajili wa Jina unalorekebisha kisha ambatanisha kwa pamoja na risiti ya malipo husika,

e) Toa Tangazo kwenye Gazeti la Serikali linalotolewa na Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali kuonyesha mabadiliko ya jina yaliyofanyika,

f) Mabadiliko yoyote ambayo hayana ushahidi wa nyaraka sahihi katika kuthibitisha maombi ya taarifa husika hayawezi kuruhusiwa/kupokelewa au kuyafanyiwa kazi na watendaji wote,

g) Mwombaji analazimika kulipia shilingi 20,000/= ikiwa ni gharama ya marekebisho ya taarifa,

h) Afisa Usajili Wilaya anaweza akaomba nyaraka nyingine yoyote atakayoona inafaa kuthibitisha taarifa/majina ya Mwombaji.

Mabadiliko kwa Wafanyakazi wa Serikali wasiotumia Mfumo wa Malipo wa Utumishi unaotumia Namba Maalumu ya Malipo ya Mshahara (Cheque Number) kwa Watumishi wa Umma

Inahusisha wafanyakazi wa Serikali wasio katika Payrol System kama vile Wanajeshi, Polisi na Taasisi zingine, Utaratibu wa kufuata ni pamoja na kuwasilisha kwenye ofisi ya Usajili ya NIDA wilayani; -

(i) Barua ya Utambulisho kutoka kwa Mwajiri wa mwombaji,

(ii) Kibali kutoka kwa Katibu Mkuu wa Wizara husika kinachotoa idhini ya mabadiliko ya taarifa kufanyika,

(iii) Cheti cha kuzaliwa kwa mabadiliko ya majina na tarehe ya kuzaliwa,

(iv) Kata hati ya kiapo cha kubadili jina (Deedpoll) toka kwa wakili anayetambuliwa na Chama cha Mawakili Tanzani (TLS) kisha kiwasilishe Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi ili kupata Usajili wa Jina unalorekebisha kisha ambatanisha kwa pamoja na risiti ya malipo husika,

(v) Toa Tangazo kwenye Gazeti la Serikali linalotolewa na Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali kuonyesha mabadiliko ya jina yaliyofanyika,

(vi) Mabadiliko yoyote ambayo hayana ushahidi wa nyaraka sahihi katika kuthibitisha maombi ya taarifa husika hayawezi kuruhusiwa/kupokelewa au kuyafanyiwa kazi na watendaji wote,

(vii) Mwombaji analazimika kulipia shilingi 20,000/= ikiwa ni gharama ya marekebisho ya taarifa,

(viii) Afisa Usajili Wilaya anaweza akaomba nyaraka nyingine yoyote atakayoona inafaa kuthibitisha taarifa/majina ya Mwombaji,



Muhimu: - ombi la mteja linaweza kuafikiwa ama lah kutegemea na sababu na nia ya mteja kutaka kufanya maboresho ya taarifa zake