emblem

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa

Jisajili, Tukutambue, Tukutambulishe
Mabadiliko ya taarifa kwa wageni wakazi/wakimbizi

Mwombaji ambaye sio raia wa Tanzania na ambaye anahitaji kubadilisha taarifa zake alizowasilisha wakati wa Utambuzi na Usajili atatakiwa kufanya mambo yafuatayo; -

(i) Kuwasilisha hati ya kusafiria,

(ii) Hati ya Mkazi halali ,

(iii) Barua ya Serikali ya Mitaa/Vijiji/Sheia aliokuwa anaishi na anakohamia kwa mabadiliko ya makazi,

(iv) Hati za utegemezi kwa wategemezi,

(v) Kiambata kinachoonyesha taarifa husika kama zilivyoandikishwa na Mamlaka za nchi anayotokea,

(vi) Nyaraka mpya inayoonyesha mabadiliko yanayotakiwa kufanyika,

(vii) Nyaraka zingine kutegemeana na kundi lake kama Mkimbizi au Mlowezi,

(viii) Kwa Wakimbizi atawasilisha nyaraka za Ukimbizi zinazotambuliwa na Idara ya Wakimbizi,

(ix) UNHCR Pamoja na barua kutoka Idara ya Wakimbizi ikiidhinisha mabadiliko husika ya taarifa zake,

(x) Kwa Walowezi; atawasilisha nyaraka za Ulowezi zinazotambuliwa na Idara ya Uhamiaji pamoja na barua kutoka ofisi hiyo ikiiridhia mabadiliko husika ya taarifa zake,

(xi) Risiti ya malipo kwa ajili ya huduma husika,

(xii) Nyaraka zingine zozote ambazo Afisa Usajili wa Wilaya atakavyoona inafaa kwa ajili ya kujiridhisha na maombi husika (Usahihi wa taarifa husika).