Marekebisho ya Majina
Mwombaji yoyote anayehitaji kufanya mabadiliko ya majina anahitajika kuwasilisha nyaraka zifuatazo:
Mabadiliko ya Majina
a) Kadi ya kliniki, tangazo, cheti cha kuzaliwa, cheti cha darasa la vii, kidato cha iv ama ‘leaving certificate’ vilivyotafutwa na wazazi awali au ulivyo viwasilisha NIDA wakati unasajiliwa na vimebeba taarifa za jina la unavyohitaji lisomeke kwa sasa,
b) Kata hati ya kiapo cha kubadili jina (Deedpoll) toka kwa wakili anayetambuliwa na Chama cha Mawakili Tanzani (TLS) kisha kiwasilishe Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi ili kupata Usajili wa Jina unalorekebisha,
c) Toa Tangazo kwenye Gazeti la Serikali linalotolewa na Mpiga Chapa Mkuu wa Serikali kuonyesha mabadiliko ya jina yaliyofanyika,
d) Afisa Usajili Wilaya anaweza akaomba nyaraka zozote zaidi ambazo ataona zinafaa kuthibitisha taarifa/majina ya mwombaji husika,
e) Mabadiliko yoyote ambayo hayana ushahidi wa nyaraka sahihi katika kuthibitisha maombi ya taarifa husika hayawezi kuruhusiwa/kupokelewa au kuyafanyiwa kazi na watendaji wote,
f) Iwapo makosa yamefanyika upande wetu, Afisa Usajili atajiridhisha na kuendelea na maboresho pasipo kulazimika kulipia gharama yoyote lah utapaswa kulipia shilingi 20,000/=,
g) Ombi la mteja litawasilishwa kwenye kamati ya Usajili na Utambuzi wa watu, iwapo watajiridhisha kuwa ombi limekidhi vigezo ndipo watatoa kibali ili Afisa Msajili aweze kuendelea na hatua ya kufanya maboresho, ombi lisipokidhi vigezo, kibali hakitatolewa na Afisa Msajili haruhusiwi kuendelea na hatua yoyote ya maboresho.
Taarifa za Maombi ya Utambulisho wa Watu zinazoruhusiwa kubadilishwa
Mwongozo wa marekebisho ya Taarifa za Usajili wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa unaelekeza juu ya taarifa zinazoruhusiwa kubadilishwa iwapo m waombaji kakidhi vigezo vya msingi vinavyo hitajika ni pamoja na; -
a) Cheti cha ndoa (Marriage certificate) cha Serikali,
b) Cheti cha talaka (Divorce certificate) cha Serikali au Nakala ya hukumu (Judment/Decree) au nyaraka ya kukaza hukumu,
c) Cheti cha kuzaliwa au Vyeti vya shule ya Msingi/Sekondari/Elimu ya juu au Cheti cha ubatizo/falaki,
d) Afisa Usajili Wilaya ili kutekeleza majukumu yake kwa usahihi anaweza akaomba nyaraka nyinginezo zozote zenye kuthibitisha taarifa/majina ya Mwombaji husika,
e) Mwombaji anapaswa kuchangia gharama ya kubadili taarifa husika shilingi 20,000/= na iwapo makosa yamefanyika upande wetu, Afisa Usajili atajiridhisha na kuendelea na maboresho pasipo kulazimika kulipia gharama yoyote,
f) Afisa Usajili Wilaya anaweza akaomba nyaraka zozote zaidi ambazo ataona zinafaa kuthibitisha taarifa/majina ya mwombaji husika,
g) Mabadiliko yoyote ambayo hayana ushahidi wa nyaraka sahihi katika kuthibitisha maombi ya taarifa husika hayawezi kuruhusiwa/kupokelewa au kufanyiwa kazi na Maafisa Usajili wilaya.
Muhimu: - ombi la mteja linaweza kuafikiwa ama lah kutegemea na sababu na nia ya mteja kutaka kufanya maboresho ya taarifa zake